Taarifa iliyotolewa na Wizara ya Ulinzi ya Russia imesema kwamba, jeshi la anga la nchi hiyo limeangamiza kambi mbili walioondoka eneo la Al-Tanf kwenye mpaka wa Syria,Iraq na Jordan na kujificha katika eneo la milimani,mashariki mwa mkoa wa Homs magharibi mwa Syria, na katika eneo la Al-Amur katika mkoa huo.
Taarifa ya Wizara ya Ulinzi ya Russia imeongeza kuwa, katika eneo la al-Tanf, kunarikodiwa kesi 9 za ukiukaji wa anga unaofanywa kila siku na ndege za kijasusi za F-15,Typhoon, Thunderbolt na MC-12W, ambazo zote ni za muungano wa Marekani eti dhidi ya ISIS.
Jeshi la Marekani liliteka baadhi ya maeneo ya Jazeera na al-Tanf nchini Syria na kuanzisha vituo vya kijeshi huko kwa ajili ya kupambana na kundi la kigaidi la ISIS
0 Comments