Bingwa wa kombe la Five Brothers Rede Competition (FBRC) msimu uliopita Mwakwani Basket Ball amefanikiwa kutetea taji hilo kwa mara nyingine baada ya kutoka kifua mbele dhidi ya Tanga kwanza.
Fainali hiyo iliyochezwa katika viwanja vya Ccm mkwakwani mkoani hapa imefanyika kwa round mbili ambapo raundi ya kwanza ilimalizika kwa Mkwakwani Basket Ball kupata ushindi wa alama 4 dhidi ya 3 za mpinzani wake Tanga kwanza.
Raundi ya pili Tanga kwanza aliukataa uteja baada ya kupambana na kulazimisha kutoka sare ya alama 3-3 ikiwa ni tofauti ya alama moja iliyomfanya Mkwakwani Basket Ball kutawadhwa kuwa bingwa wa mashindano hayo kwa msimu huu wa mwaka 2020/2021.
Mashindano hayo yalizinduliwa rasmi February 7 mwaka huu yazikihusisha timu 11za jiji la Tanga zilizoshiriki katika kinyang'anyiro hicho ambapo yamefungwa wikiendi hii na mstahiki meya wa jiji hilo ndugu Abdulhaman Shiloo ambaye ndiye aliyekuwa mgeni rasmi akiambatana na katibu tawala wa wilaya ya Tanga mjini Bi Faidha Salim.
Mashindano hayo yaliyoandaliwa na kampuni ya Five brothers yalidhaminiwa na Bank ya NMB tawi la Tanga , Anjari Drinking pamoja na Tanga Fresh ikiwa ni msimu wa tano tangu michuano hiyo izinduliwe.
0 Comments