RUANGWA WAPONGEZA ZIARA YA RAIS SAMIA

Wananchi  wa Wilaya ya Ruangwa, Mkoa wa Lindi wameonesha kupongeza jitihada mbalimbali zinazofanywa na Serikali inayoongozwa na Rais Mhe.Dkt. Samia Suluhu Hassan na ujio wake katika Wilaya hiyo umewapa faraja.

Wakazi hao wakizungumza katika nyakati tofauti leo wilayani hapo wamesema kuwa Serikali imeboresha maisha yao kwa kuwafikishia huduma mbalimbali.

Mkazi wa Kilimahewa Wilaya ya Ruangwa, Bi. Rahma Hokororo amesema kuwa ziara ya Rais Samia katika  Wilaya Ruangwa inawapa matumaini kuwa miradi mingi zaidi ya  maendeleo itatekelezwa kwa manufaa yao.

Aidha amesema kuwa huduma za afya ikiwemo za uzazi zimeendelea kuimarika na kupatikana  kwa urahisi na haraka  wilayani humo.

 Bw.Abubakar Mkwepu amesema kuwa waanamini ujio wa Mhe. Rais  utawapa fursa mbalimbali ikiwa ni pamoja na wajasiriamali kuuza bidhaa zao na wengine kuona fursa za uwekezaji zilizopo wilayani humo.

"Baadhi ya miradi imekamikika, mfano Hospitali ya Wilaya ya Ruangwa, pia kuna vituo vya afya ikiwemo  cha Mbuyuni vimekamilika na tayari vimeanza kutoa huduma kwa kweli tunampongeza na kumshukuru Rais Samia"ameeleza Bw.Mkwepu.

Ameongeza kuwa katika miradi ya elimu, kuna majengo ya kisasa katika kila kijiji na  wanafunzi wasoma katika mazingira bora.

Mhe.Rais Samia ameendelea na ziara yake katika Mkoa wa Lindi ambapo ataweka mawe ya msingi na kutembelea miradi mbalimbali ikiwemo  Hospitali ya Rufaa ya Mkoa,Shule ya Sekondari ya Wasichana Lindi,Bandari ya Uvuvi sambamba na kuzungumza na wananchi katika mkutano ya hadhara.

Post a Comment

0 Comments