takwimu za Kilimo mifugo na Uvuvi itafanyika kuanzia mwezi ujao
taarifa itakazokusanywa itaonyesha hali halisi ya sekta ya kilimo
nchini na kuiwezesha serikali kupanga sera mipango kuimarisha na
kuboresha hali za wananchi.
Kwitega ameyasema hayo wakati akifungua mafunzo ya siku tatu ya
wadadisi wa sensa ya kilimo mifugo na uvuvi ya mwaka 2019/20 kutoka
mikoa ya kanda ya kaskazini yalioandaliwa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu
inayofanyika jijini Arusha.
Alisema kuwa kwa ujumla umuhimu wa kilimo unafahamika na takwimu hizo
zitaonyesha jinsi sekta hiyo inavyochangia katika pato la taifa kwani
mwaka 2019 sekta hiyo imechangia pato la taifa kwa asilimia 26.6 huku
upande wa mauzo ya nje asilimia 24.3 ya fedha za kigeni
ilipatikana.
0 Comments