CHAMA CHA KULINDA NA KUTETEA HAKI ZA WALIMU(CHAKUHAWATA)YAPATA VIONGOZI WAPYA

Emanuel Herman Mwenyekiti wa Chama cha kulinda na kutetea haki za Walimu Tanzania (CHAKUHAWATA)akizungumza na Waandishi wa Habari mara baada ya kutangazwa matokeo ya Uchaguzi wa viongozi na kuwa mshindi.

***************

Chama cha kulinda na kutetea haki za Walimu Tanzania ( CHAKUHAWATA) kimefanya mkutano mkuu Kitaifa na Kufanya uchaguzi wa viongozi mbalimbali wa chama hicho na kumchagua Bw. Emmanuel Patric Herman kuwa Mwenyekiti wa chama hicho

Mkutano huo wa CHAKUHAWATA umefanyika Jijini Tanga ambapo wajumbe walishiriki kuchagua viongozi hao kwa kuwapigia kura ya siri huku Bw Emanuel Herman ameshinda kiti cha uenyekiti kwa kupata kura 168 na mpizani wake ambae  ndiye aliekuwa mwenyekiti aliepita Bw. Ashery Ntayomba amepata kura 106 huku jumla ya wapiga kura wote walikua ni 302

Pia chama hicho kimemchagua Rebeka Emmanuel kuwa Mwenyekiti Msaidizi na Bw. Twalb Nyamkunga  ameshinda nafasi ya Katibu Mkuu pamoja na Elias Chanda yeye ameshinda nafasi ya Muwekahazina.

Chama hicho kilianza kikiwa na wanachama 180, na mpaka kufikia 2024 chama hicho kina wanachama zaidi ya 29000

Post a Comment

0 Comments