MAFURIKO YALETA SIMANZI KILINDI

 

Wananchi mbalimbali wakiwa wamebeba
 jeneza lenye mwili wa aliyekuwa mwenyekiti wa serikali ya Kijiji cha
Mvungwe kilichopo Kata ya Songe Wilaya ya Kilindi, Juma Mnyau
wakiupeleka katika makazi yake ya milele.
Mnyau alipoteza maisha baada ya kusombwa na maji yam to Mvungwe
alipokuwa akivuka.
Picha na Dege Masoli.

Shekhe wa Kata ya Songe, iliyopo Wilaya ya Kilindi Mkoa wa Tanga, Ramadhan
Mtambi akiongoza dua mbele ya jeneza lililobeba mwili wa aliyekuwa
mwenyekiti wa serikali ya Kjiji  cha Mvungwe Kata ya Songe, Juma Mnyau
ambae alipoteza maisha kwa kusombwa na maji kwenye mto Mvungwe
alipokuwa akivuka.
Picha na Dege Masoli.

****************

Na Dege Masoli,KILINDI.

 WATU watatu wamepoteza maisha baada ya kusombwa na maji akiwemo
 mwenyekiti wa serikali ya kijiji cha Mvungwe kilichopo Kata ya Songe
 Wilaya ya Kilindi Mkoa wa Tanga Juma Mnyau.

 Kwa mujibu wa taarifa zilizopatikana eneo la tukio na kudhibitishwa na
 Kamanda wa polisi Mkoa wa Tanga,ACP Saphia Jongo ni kwamba matukio hayo
 yalitokea kwa nyakati tofauti katika Kata ya Songe kwa kipindi cha
 wiki moja.

 Sambamba na mwenyekiti huyo wengine waliyopoteza maisha  kwa mwezi huu
 wa  february ni  mkazi mmoja wa kijiji cha Kingo kilichopo Kata ya
 Songe,Erasto Mmeka na mjukuu wake ambaye hajajulikana jina walikufa
 maji.

 Kwa upande wa Kamanda Jongo  alisema tukio la mwenyekiti huyo
 lilitokea february 22 majira ya saa kumi jioni wakati alipokuwa
 akivuka mto Mvungwe akitoka nyumbani kwake  kuelekea kijijini na maji
 kumzidi nguvu na kumsomba.

 Wakizungumza na waandishi wa habari katika eneo la tukio,mashuhuda
 hao walidai kuwa Mnyau alikuwa akivuta mro huo akiwa na mkewe mdogo na
 mtoto wake wa kiume aliyetajwa kwa jina la Shaban.

 Omar Mpepo aliyedai kushuhudia  tukio hilo, alieleza kuwa  marehemu
 aliondozana na famiilia yake  na baada ya kufika kwenye mto huo alimpa
 mwanae Shaban baiskeli yake aivushe ng'ambo.

 "Unajua  Shaban  alivuka na baiskeli ile pamoja na mama yake mdogo
 (mke mdogo wa baba yake) hadi ng'ambo na wakati akirudi baada ya
 kuvusha baiskeli alirudi kuvuka na kutana na baba yake ambaye wakati
 huo alirudi  kuchukua simu yake aliyokuwa ameisahau kwa mke mkubwa"
 alisema Mpepo.

 Akieleza kuwa wakati yule kijana anavuka kurudi na kukutana na baba
 yake upande wa pili alimtahadharisha baba yake kwamba asivuke kwanza
 kwa kuwa maji alipovuka kwa mara ya pili yalionekana kuongezeka kwa
 kasi.

 Hata hivyo marehemu hakuwa na subra na badala yake aliamua kuvuka na
 wakati alipofika katikati ya mto maji yalimzidi nguvu na kumsomba na
 pamoja na kujitetea lakini haikuwa na mafanikio na hivyo kuzamishwa.

 Aidha Mussa Mangole na Salehe  Mgunga walieleza namna walivyopata
 taarifa ya simu kutoka kwa mmoja wa watoto wake kuhusu tukio na kwamba
 baada ya kufika kwenye eneo la tukio waliamua kuusaka mwili wa
 marehemu ambao ulikutwa  sehemu inayoitwa Kwangome na kuubeba hadi
 zahanati ya kijiji cha Mvungwe.

 Naye diwani wa Kata ya Songe, Abuubakari Makengwa alieleza tukio
 lingine la kijiji cha Kingo ambapo alisema mfugaji wa jamii ya kimasai
 Meka pamoja na mjukuu wake walipoteza maisha  ambapo mjukuu
 alitumbukia kwenye dimbwi la maji huku babu yaker alipigwa na mawimbi.

Na Kamanda wa Polisi mkoa wa Tanga ACP Safia Jongo amewaasa wananchi kuwa makini katika wakati huu wa mabadiliko ya hali ya hewa ambapo mvua zimekua zikinyesha.

"Watu wachukue tahadhari na ametoa takwimu za watu waliofariki kutokana na mafuriko kuanzia tarehe 11 Januari na Februari 22 ambapo jumla ya idadi ya watu waliofariki na maji kuwa jumla yake watu sita wamefariki maji katika wilaya ya Lushoto,Korogwe,Muheza,Handeni na Kilindi,na watoto wawili kutoka maafa ya maji.

Post a Comment

0 Comments