Mkurugenzi wa Uchaguzi wa TumeHuru ya Taifa ya Uchaguzi, Bw. Kailima Ramadhani alipata fursa ya kukaguabaadhi ya vituo vya uboreshaji wa Daftari la Kudumu la mpiga Kura katika Wilayaza Kasulu za Buhigwe mkoani Kigoma na kujionea hali ilivyo vituoni na mwitikiowa watu katika vituo hivyo.
Akizungumzia uboreshaji huo,Kailima alisema hadi kufikia jana tarehe21 Julai 2024, hapakua na changamoto yeyote iliyojitokeza katika mikoa yote yaTabora, Kigoma na Katavi na wananchi wameendelea kujitokeza kwa wingikujiandikisha lakini pia kuboresha taarifa zao.
Aidha Kailima alivipongezavyama kwa kuweka mawakala katika vituo vya uandikishaji na kuwataka mawakalahao kusaidia utambuzi kwa watu wasio raia wa Tanzania ambao watafika kwaajiliya kuandikishwa.
Kailima alitumia nafasi hiyokuwakumbusha wananchi kuwa sasa zimesalia siku tano kati ya saba zilizopangwa kuandikishawananchi katika mikoa hiyo ya Kigoma, Katavi na Tabora hivyo wananchi wazitumiesiku zilizobaki kujitokeza na kujiandikisha.
Amesema vyama vya siasavinawajibu wa kuwahimiza, wanachama,wapenzi na wafuasi wao kujitokeza kujiandikisha na kuboreshataarifa zao ili waweze kupiga kura katika uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025.
0 Comments