MAHAKAMA YA KIJESHI DRC YAWAHUKUMU ADHABU YA KIFO

Mahakama ya kijeshi nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imewahukumu adhabu ya kifo watuhumiwa 51 waliokabiliwa na kesi ya mauaji ya wataalamu wawili wa Umoja wa Mataifa waliouawa mwaka 2017.

Idadi kubwa ya watu walikuwa wakifuatilia kesi hiyo mahakamani tangu ilipoanza kusikilizwa zaidi ya miaka minne iliyopita. Michael Sharp, raia wa Marekani na Zaida Catalan raia wa Sweden na Chile, walikuwa wakichunguza machafuko katika mkoa wa Kasai, chini ya Umoja wa Mataifa.

Uchunguzi wao ulijikita kwenye makaburi ya halaiki yanayohusishwa na mzozo wa umwagaji damu ambao ulikuwa umepamba moto kati ya serikali na kundi la waasi la Kamwina Msapu katika mkoa wa Kasai.

Watalamu hao wa Umoja wa Mataifa walipotea na kisha miili yao ilipatikana katika kijiji kimoja mnamo Machi 28, mwaka 2017, siku 16 baada ya kutoweka. Mtaalamu Zaida Catalan alikuwa amekatwa kichwa.

Mauaji hayo ya wataalamu wawili wa Umoja wa Mataifa yaliitikisa jamii ya wanadiplomasia na wafadhili na serikali ya Kongo imelilaumu kundi la Kamwina Msapu kwa mauaji hayo.

Waendesha mashtaka katika mahakama ya kijeshi ya Kananga walipendekeza hukumu ya kifo dhidi ya washtakiwa 51 kati ya washtakiwa 54. Watuhumiwa 22 wamehukumiwa bila kuwepo mahakamani hapo kwa sababu wametoroka kutoka nchini Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Post a Comment

1 Comments

  1. youtube.com ▷ youtube.com - VideoODl
    youtube.com Videos of Video of Video of Video of Video of Video of Video of Video Video of youtube mp3 Video of Video of Video of Video of Video of Video of Video of Video of Video of Video

    ReplyDelete